Na Mwandishi Maalum, Dar Es Salaam.
Rais Jakaya Kikwete amesema uwekezaji barani Afrika unatakiwa kupunguza na hatimaye kumaliza tatizo la umasikini.
Amesemahilolitafanikiwa kwa kuongeza uwezo wa watu kupata chakula cha uhakika na pia kupata ajira za uhakika.
Rais Kikwete amebainisha hayo wakati akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Umoja wa Biashara katika nchi wanachama wa jumuiya ya madola, Dokta Mohan Kaul.
Viongozi hao wako mjini Perthnchini Australiakuhudhuria mkutano wa viongozi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola –Chogm.
Rais Kikwete amesema sasa ni wakati kwa nchi tajiri ndani ya jumuiya ya madola kuzisaidia nchi masikini katika kuwekeza zaidi.
Mwisho










