The Sound Of Africa
Saturday May 19th 2012

Interesting Sites

Insider

Archives

Vyama vya siasa 158 kukutana Nairobi.

 Na Mwandishi Maalum, Arusha.

 

Vyama vya siasa 158 kutoka nchi wananchama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki vinatarajiwa kuhudhuria mkutano wa kwanza jijini  Nairobi Kenya  kuanzia septemba 15 mwaka huu.

 

Naibu Katibu Mkuu wa jumuiya hiyo  anayeshughulikia shirikisho la kisiasa, Beatrice Kiraso amesema  vyama hivyo vina jukumu  la kuhamasisha  ushirikiano wa kiuchumi na kisiasa.

 

Amesema  mkutano huo utatoa nafasi  kwa vyama husika kuchunguza ilani zao na kupendekeza njia zitakazowezesha kushiriki katika siasa za kanda  ya Afrika Mashariki.

 

Mambo mengine yatakayojadiliwa  katika  mkutano huo ni pamoja na  usajili, demokrasia ndani ya vyama vya siasa, na jinsi ya  kukuza  amani na utulivu katika jumuiya hiyo.

 

 

Mwisho.

Related posts:

Related Ways to Take Action:
Powered by Social Actions

Leave a Reply