The Sound Of Africa
Saturday May 19th 2012

Interesting Sites

Insider

Archives

Hakielimu yatoa nakala elfu ishirini za katiba.

Na Jovita  Kaijage, Dodoma.

 

Shirika  la Hakielimu la  jijini Dar-es- salaam limetoa nakala  elfu  ishirini za katiba  zenye thamani ya  shilingi milioni 19 kwa  wananchi na taasisi mbali mbali nchini.

 

Nakala hizo zimetolewa katika  kipindi cha  kuanzia mwezi mei mwaka huu hadi sasa.

 

Hayo yamesemwa mwishoni mwa wiki iliyopita  na Mkurugenzi wa  shirika hilo Bi. Elizabelt  Missokia  wakati akizungumza katika  mkutano mkuu wa mwaka wa marafiki wa elimu  kutoka mikoa ya tanzania bara mjini Dodoma.

 

Amesema mbali na shirika  hilo kuendelea  kuwajengea uwezo  wanaharakati wa masuala mbali mbali hapa nchini  wanatambua kuwa  moja ya nyenzo muhimu wanazotakiwa kuwa nazo ni katiba.

 

Amefafanua kuwa idadi kubwa ya wananchi wanashindwa kutimiza wajibu wao kwakuwa hawatambui  haki na wajibu wao.

 

Shirika la Hakielimu lililoanzishwa mwaka 2001 likiwa na  watu 13 hivi sasa  lina marafiki wa elimu  35,353 nchini kote.

Mwisho

Related posts:

Related Ways to Take Action:
Powered by Social Actions

Leave a Reply