Na Seda Elias na Deborah Mpagama, Dodoma
Serikali kwa kushirikiana na benki ya dunia na jamii ipo katika mchakato wa utekelezaji wa miradi ya maji katika vijiji vya Dodoma.
Naibu Waziri wa Tamisemi Mheshimiwa Agrey Mwary amesema hay0 wakati akijibu swali la Mbunge David Mchiwa Malole.
Amesema utafiti wa maji na ardhi umeshafanyika pamoja na uchimbaji wa visima na vipimo vya wingi wa maji.
Amefafanua kuwa fedha za miradi hiyo zilitengwa katika bajeti ya mwaka 2010 – 2011.
Aidha katika mwaka wa fedha wa 2011 – 2012 serikali kupitia halmashauri ya manispaa ya Dodoma imeweka kipaumbele katika kuboresha kilimo cha mbogamboga katika Halmashauri hiyo kwa kujenga kuta za kinga maji kwenye mito ya msimu.
Wakati huo huo serikali imesema kuwa kwa sasa haitajenga barabara kutoka Namanyere hadi Karando mkoani Rukwa kwa kiwango cha lami
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa John Magufuli amesema hayo wakati akijibu swali bungeni leo mjini Dodoma.
Amesema kuwa katika mkoa wa Rukwa kwa sasa kuna barabara nyingi ambazo zinatengenezwa kwa kiwango cha lami.
Mwisho.










